Friday, March 29, 2024

IJUMAA KUU NJEMA

 

Tunawatakia Ijumaa Kuu Njema.⛪

Luka 23:41 Yesu akalia kwa sauti kubwa: “Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu” 🔔🕯️⛪

Monday, April 30, 2018

MBUNGE CHADEMA ALALAMIKIA VITI BUNGENI, ADAI KUFINYWA MAKALIO

Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (Chadema) ameomba mwongozo bungeni akitaka viti vya bungeni kukarabatiwa kwa kuwa viti hivyo ni vibovu.

“Ni lini serikali itakarabati viti hivi, hiki nilichokalia leo asubuhi kimenifinya makalio,“ alihoji Selasini.

Salasini ameyasema hayo leo Bungeni mjini Dodoma, wakati wa kipindi cha Maswali na majibu huku akiitaka serikali itoe majibu ni lini viti hivyo vitakarabatiwa.

Aidha Mbunge huyo baada ya kuhoji amesema kuwa kiti alichokalia leo katika bunge hilo kimemfinya makalio. Sambamba na kuomba muongozo huo Spika Ngudai amesema kuwa suala hilo limepokea na litatolewa ufafanuzi.

MAJIBU YA RAIS MAGUFULI KWA WANAOBEZA NCHI KUKOPA

Rais John Magufuli amesema Serikali itaendelea kukopa kwa ajili ya miradi ya maendeleo, hata kama kuna watu wanabeza.

Amesema fedha hukopwa kwa masharti nafuu, riba ndogo na hulipwa kwa muda mrefu na kwamba fedha hizo ndizo hutumika kujenga miundombinu kama barabara ili kuchochea uchumi.

Rais alisema hayo jana mjini Iringa alipofungua barabara ya lami ya Iringa – Migoli – Fufu yenye urefu wa kilomita 189 inayounganisha mikoa ya Iringa na Dodoma. Tukio hilo lilirushwa hewani moja kwa moja na kituo cha televisheni cha TBC 1.

Barabara hiyo iliyojengwa kwa gharama ya Sh207.4 bilioni ni sehemu ya barabara kuu ya kuanzia Cape Town, Afrika Kusini hadi Cairo nchini Misri.

Imejengwa kwa ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa asilimia 65.9, Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (Jica) kwa asilimia 21.3 na Serikali ya Tanzania asilimia 12.8.

“Msiwasikilize wanaosema Serikali ina madeni makubwa wakati wao wenyewe wanapita kwenda bungeni kwenye barabarani tulizozijenga kwa kukopa,” alisema.

Magufuli alisema Serikali imekuwa ikidaiwa tangu enzi za mkoloni, lakini madeni mengine yamekuja kulipwa katika utawala wa Rais Jakaya Kikwete.

Akizungumzia barabara hiyo, Rais alisema inalenga la kuimarisha utalii katika ukanda wa kusini.

“Watu walizoea (kwamba) ukitaka kutalii ni lazima uende Serengeti wakati Ruaha ni mbuga kubwa yenye vivutio bora, lakini haikutembelewa na watalii kwa sababu ya ukosefu wa barabara,” alisema.

“Kwa sasa itabidi wenzetu wa kaskazini wasubiri kwanza. Kwa sasa tunaendeleza maeneo yaliyochelewa kuendelezwa,” alisema.

Rais Magufuli alisema Uwanja wa Ndege wa Nduli uliopo Iringa utaimarishwa ili watalii waweze kufika maeneo ya utalii.

Rais Magufuli alisema barabara hiyo pia itawasaidia wakazi wa Iringa kusafirisha mazao kwenda sokoni bila matatizo.

“Barabara hii iwe mkombozi wa maisha yetu. Tuitunze, itasafirisha mazao, mtasafiri kwa utulivu kwenda kwenye shughuli zenu,” alisema.

Magufuli ambaye alisoma Shule ya Sekondari Mkwawa mkoani Iringa kuanzia mwaka 1978/79, alisema anakumbuka hali ya barabara ilivyokuwa tatizo wakati huo.

“Kutoka Dodoma hadi Iringa nilitumia siku mbili kwa kutumia basi la Shirika la Reli Tanzania. Tulilala njiani kwa sababu ya ubovu wa barabara,” alisema.

MCHUNGAJI KKKT ADAI KUNA UBABE KATIKA KANISA HILO

Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kigogo, Richard Hananja amedai kuna ubabe katika kanisa hilo.

Hata hivyo, amesema licha ya kanisa hilo kupitia mambo mengi anaamini litaendelea kusimama imara hasa katika kipindi hiki.

Mchungaji Hananja amesema hayo Aprili 29, 2018 alipozungumza na Mwananchi kuhusu baraza la maaskofu wa KKKT ‘kuwatenga’ maaskofu watatu kwa kutosoma waraka wa ujumbe wa Pasaka kwenye dayosisi zao.

SERENGETI BOYS MABINGWA WA CECAFA

Timu ya Tanzania ya vijana wasiozidi umri wa miaka 17 Serengeti Boys ndio mabingwa wa Kombe la Vijana la mataifa ya Afrika Mashariki na Kati Cecafa wa mwaka 2018.

Serengeti Boys walitwaa ubingwa baada ya kuwalaza Somalia mabao 2-0 katika mechi ya fainali iliyochezewa mjini Bujumbura, Burundi. Mabao ya Serengeti yalitiwa kimiani na Edson Jeremiah na Japhary Mtoo.

Ushindi huo ndio wa kwanza tangu kuanzishwa kwa michuano hiyo mwaka 2007 na unatarajiwa kuwatia moyo vijana hao wanapijiandaa kushindi michuano ya Kombe la Vijana Mabingwa Afrika mwaka 2019.

Sunday, April 29, 2018

SERIKALI YAINGILIA KATI MATIBABU YA MZEE MAJUTO, SASA KUPELEKWA INDIA, WADAU NAO WAJITOKEZA

Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison G. Mwakyembe (Mb) jana Aprili 28, 2018 amemtembelea msanii nguli wa filamu Bw. Amri Athumani (Mzee Majuto) ambaye alikuwa amelazwa kwenye Hospitali ya Tumaini, Dar es Salaam. 

Dkt. Mwakyembe akizungumza katika tukio hilo amesema Serikali imeamua kumpeleka Mzee Majuto nchini India kwa ajili kupata matibabu zaidi. 


"Kwa kuanzia tumeamua kumuhamishia Mzee Majuto katika hospitali ya Muhimbili ili kukamilisha maandalizi muhimu ya kiafya kabla ya safari ya kuelekea India", alisema Dkt. Mwakyembe.

Thursday, April 26, 2018

NENO LA MIZENGO PINDA KUHUSU WATU WAOFANYA VURUGU NCHINI

Waziri Mkuu mstaafu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Mizengo Kayanza Peter Pinda.
Hii ilikua Juni 20, 2013, akizungumza katika Kipindi cha Maswali ya Papo kwa Hapo kwa Waziri Mkuu, bungeni Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa Kilwa Kaskazini Murtaza Mangungu .

Mh. Pinda alisema “Ukifanya fujo umeambiwa usifanye hiki ukaamua wewe kukaidi utapigwa tu maana hakuna namna nyingine maana wote lazima tukubaliane nchi hii tunaiendesha kwa misingi ya kisheria sasa kama wewe umekaidi hutaki unaona kwamba ni imara zaidi, wewe ndio jeuri zaidi watakupiga tu na mimi nasema muwapige tu, kwa sababu hakuna namna nyingine maana tumechoka sasa”.

HISTORIA YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR


Mkataba wa Muungano ulitiwa saini na Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Amani Karume, Aprili 22, 1964, Zanzibar.
Ulithibitishwa na Bunge la Tanganyika na Baraza la Mapinduzi Aprili 26, 1964, na Aprili 27, 1964 viongozi hao walikutana katika ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Dalaam kubadilishana hati za Muungano.


Sheria za Muungano ilitamka kwamba, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar zililazimika, kuwa dola ya Jamhuri kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, jina ambalo lilibadilishwa Oktoba 28, 1964 na kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupitia sheria ya Jamhuri ya Muungano, sheria namba 61, ya mwaka 1964.

Wednesday, April 25, 2018

ALICHOSEMA KAMANDA WA POLISI DODOMA KUHUSU MAANDAMANO YA KESHO

Bofya hapo chini upate kusikiliza kauli ya kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma Gilles Muroto kuhusu maandamano ya kesho. Usisahau ku-subscribe, kulike na kucomment.

Thursday, April 19, 2018

BABU SEYA NA WANAE WATINGA BUNGENI LEO

Mwanamuziki nguli wa dansi, Nguza Viking ‘Babu Seya’ na watoto wake ambao ni Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ na Francis Nguza, leo Aprili 19, 2018 wametembelea Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma baada ya kualikwa na Mbunge wa Viti Maalum CCM, Mariam Ditopile.

Babu Seya na familia yake, walishangiliwa na Bunge zima baada ya kutambulishwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai, baada ya kipindi cha maswali na majibu kumalizika bungeni humo.

Wanamuziki hao walikuwa ni miongoni mwa wafungwa 8,157 waliosamehewa na Rais John Magufuli siku ya maadhimisho ya sherehe za uhuru wa Tanganyika, Desemba 9, 2017 zilizofanyika mjini Dodoma.

MSUKUMA 'LEMA SASA HIVI KIDOGO AMEKUWA BINADAMU'

Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Msukuma, amemuomba Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi, kupeleka bungeni muswada  kubadilisha sheria ili makosa ambayo hayastahili mtu kufungwa apewe adhabu ndogo ili kuondoa msongamano katika magereza.

Pia mbunge huyo aliwataka baadhi ya wabunge waache kupiga kelele bungeni juu ya matukio ya watu kupotea na kutekwa, badala yake waviache vyombo vya sheria na vya usalama vifanye kazi yake.

Hayo ameyasema Bungeni wakati akichangia hoja katika Wizara ya Katiba na Sheria jana, Aprili 18, 2018.

PICHA ZA HARUSI YA ALIKIBA ILIYOFANYIKA MOMBASA



 Baada ya ukimya na usiri wa muda mrefu kuhusu mahusiano yake ya kimapenzi hatimae leo April 19, 2018 Ali kiba amefunga ndoa katika msikiti wa Ummul Kulthum Mombasa nchini Kenya akiwa ameozeshwa na sheikh Mohammed Kagera.


Alikiba  amemuoa Amina Khalef Ahmed mkazi wa Mombasa ambapo ndipo sherehe za harusi hiyo zinafanyika hii leo huku sherehe nyingine kubwa ikitarajiwa kufanyika April 29, 2018 jijini Dar es Salaam.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...